MIND POLLUTION. - EMAGK SITE

Latest

This website was designed to help college student especially those who takes engineering course for review, past paper and other learning material. And teacher for review.

Monday, November 8, 2021

MIND POLLUTION.

 



THE MIND 
POLLUTION 
Uchafuzi Waakili

 

UCHAFUZI WAAKILI (MIND POLLUTION)... 19April2019

Utangulizi


Mind pollution: ni kati ya vitu hatari sana hapa duniani, unashangaa mtu anakusifia leo kesho anakuwa wa kwanza kukupiga mawe. na aliekuwa hakuelewi ndio anaekusaidia. 
aina hii ya uchafuzi ndio aina mbaya na ugonjwa mbaya zaidi wa akili hapa duniani kwa maendeleo ya mtu binafsi, taasisi, nchi na dunia kwa ujumla.
Matendo 14:1-3 verse “But the unbelieving jews stirred up the Gentiles and poisoned their minds against the brothers.”(translation from English standard version). 
 
 Matatizo yote tunayoyaona huwa yaanzia kwenye akili, kuna kitu nakiita mind pollution au uchafuzi wa akili, kama ilivyo uchafuzi wa mazingira ni hataria kwa afya ya mwanadamu na  viumbe hai ndivy ilivyo mind pollution (uchafuzi wa akili) ni hatari Zaidi maana ndio chanzo cha uchafuzi na chochote kibovu na kiovu tunachokiona. Embu tuangalia hiii ni nini? Bibilia inasema nini juu yah iii?

 

 

Uchafuzi Wa AKILI (Mind pollution) ni nini?

 

Uchafuzi wa akili Ni kuwepo kwa taarifa ambazo sisahihi kwenye ufahamu au akili ya MTU. Taarifa hizi huanza kubadilisha namna ya MTU anavyowaza anavyofikiri  na hata namna ya kuongea na matendo yake huanza kubadilika  kwa namna ambae hata yeye anaweza asitambue kwamba ameanza kutoka  kwenye mstari uliosahihi. Mabadiliko haya yanaweza kuchukua miaka kadhaa  kwa MTU kubadilika kabisa. Hapa ndipo naweza ukashangaa kukutana na  MTU ambae alikua anachukia kitu Fulani na kukipiga vita lakini Leo anakifanya  na kukitetea kwamba ni sahihi. Mfalme sulemani aliangukia kwenye mtego  huu. Mtu ambae alipinga sana ibaada za sanamu mwisho moyo wake unageuzwa wakatiwa uzee wake na kuanza kuabudu sanamu.(1falme 11:1-3). Mind pollution (uchafuzi wa akili) ni hatari sana kuliko unavyofikiri. Maana hii


Haijali mtoto, kijana wala mzee, wala haijali unahekima au la.. karibu tujifunze  pamoja 
 
Uchafu ni nini?

 

Uchafu ni taarifa yoyote ile ambayo IPO  kinyume na taarifa sahihi. (kweli). Huo ni uchafu.Taarifa yeyote ambayo haichangii chochote kile kwenye maendeleo yako ya kiuchumi, kijamii na kiroho huo ni uchafuzi.Umbea, kusengenya, nakusikiliza chochote kile ambacho akikusaidii kukua  kwenye Nyanja hizi nne muhimu yaani kiafya, kijamii, kiroho na kiuchumi huo ni uchafuzi.

 

Taarifa zozote zile ambazo zinabomoa ndoa yako huo ni uchafu.Taarifa yoyote ile ambayo inakuvunja moyo au kukutia hofu kwenye jambo la msingi unalotaka kufanya huo nao ni uchafu. Taarifa zozote zile zinazokutenga na Mungu, huo nao ni uchafu, haijalishi amesema nani, umeangalia wapi, au watu wangapi wanasapoti. Vijana wengi wamearibika kwasababu ya uwepo Wa taarifa nyingi ambazo ni hasi, watoto wanaharibika na kuwa na tabia mbaya kwasababu ya taarifa mbaya anazopata kupitia muvi, mziki, YouTube na n.k.Taarifa za kweli pekee ndizo zinazoweza kumfanya MTU akue vizuri na awe mwenye furaha na mafanikio kwenye Nyanja zote. 
 
 JE TATAMBUAJE TAARIFA ZA KWELI?
 
Mwenye taarifa sahihi ni mtengenezaji Wa kitu hicho. Mara nyingi watengenezaji hutoa taarifa ya namna ya kutumia na kutengeneza chombo  hicho ikiwa kimeharibika ijulikanayo kama USER MANNUAL BOOK. Dunia na vyote viijazavyo vinavyoonekana na visivyoonekana vimeumbwa na Mungu. Hivyo  MUNGU ndie mwenye taarifa sahihi kuhusu  vitu vyote vya duniani na mbinguni. Mwenye taarifa sahihi kuhusu wewe na vitu vinavyo kuzunguka ni Mungu Pekee. Lakini pia Mungu ametupa User Manual  (kitabu chenye taarifa sahihi)  yaani BIBLIA. Taarifa zozote ambazo zipo  kinyume na neno la Mungu au taarifa alietoa Mungu huo niuchafu..1 Wakorinto:10.26, Mwanzo1:1, zaburi24:1.Lakinipia fahamu hilikila kitu kimetengenezwa kwa kanunina iliupate matokeo ulio haidiwa nilazima ufuate kanuni, na kanuni hizo ni moja ya taarifa sahihi ambazo zinapatikana kwa mtengenezaji pamoja na User Manual (kitabu chenye Maelezo ya namna ya kutumia na taarifa zote za muhimu) alietoa. 
Na  ukienda kinyume na taarifa alie toa mtengenezaji kamwe huwezi kupata matokeo aliyokuahidi. 
 
Pia fahamu hili taarifa yeyote yenye ukweli asilimilia 99% na uongo 1% uwe na uhakika hizo taarifa siyo sahihi.Kama nilivyosema mwanzo kila kitu kimetengenezwa kwa kanuni hivyo ukivunja kanuni hata moja huwezi pata Matokeo yaliokusudiwa na hii Ndio sababu Biblia inasema ukivunja sharia  moja umevunja zote maana kanuni zote zipo kwenye hicho kitu kimoja na zimewekwa na mtengenezaji. Yakobo2:10

Mfano:

Siku moja nikiwa napita maeneo Fulani nilikuta sehemu moja wana uza taa za umeme. Kwa Maelezo yamuuzaji taa hizo zina tumika kwenye umeme Wa nyumbani ujulikanao kama  UMEME WA TANESCO. Basi nikachukua taa hiyo  na kwenda Nayo nyumbani, nilipofika niliiweka taa hiyo na kuwasha swichi yangu ya umeme. Baada ya kuwasha tu swichi taa ile ililipuka SAA hiyo hiyo. Haraka nikachukua kasha ambayo iliwekwa humo ilikuangalia  maelekezo ya mtengenezaji, nilipoiangalia nikagundua ilikuwa ni taa ya solar volt12, na  Mimi nimeiweka kwenye umeme Wa volt Zaidi 200. Nikaishia kupata matokeo  ambayo sikutarajia

FAHAMU  HAYA:

1. Hutapata matokeo yaliyokusudiwa na mtengenezaji kama ukivunja kanuni mojawapo ya zile alizoziweka kwasababu zozote zile hata kama hahukujua, ulidanganywa au hakupata taarifa zote.2.Taarifa zote unazopewa uwe na mazoea ya kizipima na taarifa ya mtengenezaji( usermanual). 
 
Kwanini uzipime? 
 
Mtoa taarifa anaweza akawa anaangalia maslahi yake bila kujali matokeo utakayopata. 
Au Amesahahu au hakuelewa vizuriau hakusoma kabisa taarifa ya mtengenezaji na anatumia uzoefu kutokana na vile alivyosikia au kufundishwa. Weka hii akilini kila taarifa unayopewa ipime na taarifa ya mtengenezaji. Vinginevyo utamlalamikia mtengenezaji kwa kupata matokeo hasi (negative) kwa uvivu wako Wa kutokusoma taarifa alizozitoa.

Fahamu ili.

Taarifa zote muhimu za kukuhusu wewe na vitu vinavyokuzunguka vinapatikana kwenye BIBLIA ambayo ndiyo user manual tuliopewa.. Usiiamini taarifa yeyote inayopingana na Neno la Mungu yaani Biblia.. Hata kama inatoka kwa kiongozi Mkubwa na unaemwamini sana. Usimwamini MTU yeyote kupita unavyo mwamini Mungu.Uwe na tabia ya kuisoma Biblia yako ili uweze kupambanua taarifa sahihi na ile isiyo sahihi.

VYANZO VYA TAARIFA

Taarifa zote sahihi na za kweli zinatoka kwa Mungu pekee na si kwingineko Chanzo cha taarifa zote za uongo ni shetani na yeye ndie baba Wabongo. Lengo lake kubwa ni kuharibu    na kutuweka mbali na Mungu ili aweze kutuchezea, kutuharibu na kutuangamiza kabisa.

 

Fahamu ili.

Pia ana uwezo Mkubwa Wa kumshawishi na kumdanganya MTU iliafuate uongo wake hasa asiekuwa na hiyo kweli ya Mungu.


Na ndomaana hata Yesu mwenyewe alivyojaribiwa alimshinda  Kwaneno (kweli) ya Mungu 
 
Taarifa unazoangalia you tube, muvi unazoangalia, mziki, majarida unayosoma,genge unalokaa, maarifiki ulokuwa nao, Je wanakujenga au wanakuboa kwa taarifa zao? Kwasababu shetani huwekeza kwa MTU taarifa hasi na Mungu huwekeza  taarifa chanya kwa watu pia,hivyo kuwa maakini na hadithi mnazo piga pamoja na taarifa unazopata.

 

 

NAMNA YA KUJILINDA NA MIND POLLUTION: 
Biblia imeweka wazi namna yakuepuka tatizo hill. Hata kabla ya mfalme sulemani Mungu alitoa mausia juu ya hili. Hebu tuangalie mistari michache ya Biblia Mungu aliwaambia wana Wa Israeli wasioe MTU Wa mataifa wasije wakageuzwa mioyo yao ielekee Baali.(Kumb7:2-5,kumb17:14-20)Sulemani pamoja na hekima alivunja mausia haya na mwishoni moyo wake uligeuzwa na kuanza kuabudu miungu mingine.(1falme11:1-3)Hii inaonyesha wazi Mungu alifahamu nguvu ya taarifa unazozipata kila siku zinauwezo Mkubwa  Wa kumbadilisha MTU haijalishi anamfahamu Mungu kiasi gani au ana hekima kiasi gani.Lazima uifahamu kweliYesu akasema mtaifahamu kweli na hiyo kweli itawaweka huru. Kuwa na taarifa sahihi kutakupa uwezo Wakupambanua taarifa za uongo. Taarifa yenye ukweli asilimia99% na uongo asilimia1% inahitaji MTU mwenye uelewa  Mkubwa juu ya hiyo kweli ilikubaini uongo huo, na kujua kua taarifa hiyo si sahihi. Na hii Ndio sababu Mungu akatupa user manual (Biblia) ili kila taarifa 
 
1.tunayoipata tuipime kwa hiyo. Sasa hutaweza kupima kama huifahamu hiyo  kweli.Weka kila jitihada kuifahamu kweli yaani neon la Mungu (Biblia). 
 
2.Ufuate mausia ya Mungu. 
 
3.Usiketi baradhani pawenye midhaa.. Zaburi1:1- 
 
4.Uwe na marafiki mwenye hekima (wazuri). 
 
5.Soma na kulitafakari neon la Mungu. Yoshua1:8 
 
6.Tafakarini mambo yoyote yaliyo mema.(Filipi4:8, Efeso4:16) 
 
7.Kesheni mkiomba...Luka11:36

 

 

 

MADHARA YA UCHAFUZI WA AKILI. (MIND POLLUTION) 
Taarifa zote ambazo ni hasi zinakutoa kwenye kweli na kukuingiza kwenye hatia. Taarifa hizi huzuia mafanikio ya mtu katka Nyanja zote.

 

Fahamu hili hatma ya taarifa hasi (mind pollution) ni mauti.


 

Hebu angalia. 
Kwa Mara ya kwanza mind pollution ilitokea pale bustanini mwa edeni, baada ya hawa (Eva) kuziamini taarifaa mbazo ziko kinyume na zile alizotoa Mungu. Hapa ndipo chanzo cha mwanadamu kutenda kinyume na Mungu. Na Mara nyingi taarifa hasi zinaweza kuja na ahadi nyingi ambao mwisho wake ni mauti. Adamu na Hawa walipoenda kinyume na taarifa alietoa Mungu hawakupata Yale matokeo ambayo shetani aliwaambia Bali Yale ambayo Mungu aliwaambia.(hakika mtakufa).Wana Wa Israel walipoenda kinyume na taarifa alizotoa Mungu waliangukia utumwani. 
 
Paulo akasema sisije tutapataje kupona tusipojali wokovu mkuu namna hii? Luka:13.3 Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.

 

Ezekieli:18.4 Tazama, roho zote ni mali yangu; kama vile roho ya baba ni mali yangu, ndivyo ilivyo roho ya mwana mali yangu; roho ile itendayo dhambi itakufa. Nimalizie Kwa kusema hivi wale waliotumwa kuipeleleza yeriko kati ya watu kumi na mbili ni watu wawili tu walioleta taarifa njema ila kumi wote walileta taarifa mbaya mbele ya wana Wa Israel na mwisho wana Wa Israel wa kaamini taarifa za wale kumi ambazo zilikuwa kinyume na Mungu, hata ikazua ugomvi na watu wengi kupoteza maisha na kushindwa kufika kule ambako Mungu alikusudia kuwafikisha. Kuna wakati mwingine hatujafika mahali ambako Mungu amekusudia kiuchumi ,jamii, kiroho hata kimwili kwasababu ya mind pollution(taarifa hasi tulizopata na kuziamini). Weka bidii ya kutafuta na kuamini taarifa za kweli.

 

NAMNA YA KUONDOA ATHARI ILIYOSABABISHWA NA UCHAFUZI WA AKILI:Cha kwanza ambacho ni muhimu ni lazima uondoe kwanza taarifa zote  ambazo sisahihi zilizoleta madhara kwenye maisha yako. Nakuzireplace na taarifa sahihi. Lakini pia tambua hili:- 
 
Taarifa hasi ni rahisi sana kumwingia mtu na kuacha athari kwenye maisha yake. Kama ilivyo ni rahisi kuchafua kuliko kusafisha. 
Ningumu sana kwa taarifa hasi kuondoka, inahitajika gharama, kama ilivyo  kusafisha ni gharama, pia kusafisha akili, kuondoa huo uchafu kwenye akili kuna gharama.

 

Chagua kuziamini, kuzitii na kuzifuata taarifa za Mungu bila kujali wengi wanasema nini. 
Kisha,.. 
1.Kaa mbali na vyanzo vya taarifa hasi, 
2.Fanya bidii kusikiliza, kuangalia au kusoma taarifa sahihi, zitafakari na kuziamini 
 
Mind pollution inamplekea mtu kutenda dhambi, na dhambii na mtenganisha  mtu na Mungu.Yesu alikufa msalabani ilikurudisha   kutupatanisha na Mungu, maana uhusiano wetu uliharibiwa na dhambia mbayo chanzo chake ni baada ya adamu na Haaa kuamini taarifa hasi zilizoletwa na shetani. Ashukuriwe Mungu kwamaana Kwa kumuamini Yesu kristo madhara yote na  vifungo vyote vilivyosababishwa na mind pollution zina safishwa na kutuacha  huru kabisa. Huku tukivikwa uwezo Wakuishi sawa sawa na makusudi ya Mungu. 
 
Maisha yenye furaha na mafanikio halisi yanapatikana ndani ya wokovu. Fanya maamuzi sasa.Maisha bila Mungu ni sawa na chai yenye viungo vyote karafuu, iliki, n.k lakini ikakosa sukari. Hakika nakuambia hatakama inanukia kiasi gani hainyweki ukipeleka mdomoni utatema tu. Ni sawa na maisha ya mtu mwenye kila kitu akamkosa MUNGU.  
 
Lakini pia kumbuka chai ni nzuri inapokuwa ya moto ikipoa tu hau taweza kuitumia, ndivyo ilivyo Kwa maisha ya mtu alieokoka, uliitwa na kusafishwa ukaokolewa ilipia uwe mtakatifu kama Baba (MUNGU) alivyomtakatifu. Kuna wengine hawaeleweki mambo wanayofanya, wengine wanaangalia X na mambo mengi ambayo hata katika jamii tu hayafai. Wengine wanavaa mavazi ambayo hata jamii inashindwa kuwaelewa, wamekuwa kama chai iliyopoa  hainyweki sasa ndungu yangu sibora ungebakikuwa Maji maana Maji ya baridi yananyweka vizuri.

Iliuendelee kuwa moto hakikisha unasoma na kutafakari Biblia, unaomba Mara tatu Kwa siku, na kufunga angalau Mara moja Kwa wiki na kuyaishi Yale ambayo Mungu anasema na wewe.Kama unapata shida kwenye usomaji Wa Biblia. Unaweza kujiunga na magrup mbalimbali yatakayokusaidia kujisomea Biblia yako mwenyewe. Kama BIBLE  RACE2 019, NA Gospel unlimited fellowship 

 

 

 

Imeandaliwa na 

Emanuel Israel kangala

 +255742859313

Baruapepe: emanuelkangala@gmail.com

19April2019

2 comments: