THE TRUTH YOU HAVE TO KNOW ABOUT TALENTS AND SPIRITUAL GIFT - EMAGK SITE

Latest

This website was designed to help college student especially those who takes engineering course for review, past paper and other learning material. And teacher for review.

Tuesday, March 5, 2024

THE TRUTH YOU HAVE TO KNOW ABOUT TALENTS AND SPIRITUAL GIFT

 


 

 Chochote ambacho MUNGU ameweka kwako sio chako ni kwaajili ya watu na jamii inayokuzunguka, Sio kwafaida yako ni kwa faida ya wengine, Hii hamaanishi kwamba wewe ni wa muhimu sana kushinda wao, la hasha bali umeaminiwa kupewa ulichopewa kuwa utakifikisha kwa watu waliokusudiwa kwa namna sahihi, muda sahihi, ilimfae kila mmoja aliekusudiwa.

Kila mmoja ni wa muhimu, do you know why? Kila mmoja amebeba kitu cha pekee kwaajili ya faida ya wengine. Ukiidharau cha mwenzako umedharau na kuicheka kesho yako. Maana sio kwaajili yake amepewa kwaajili ya mapungufu uliyonayo.

1korintho 12:4 BASI PANA TOFAUTI YA KARAMA, BALI ROHO NI YEYE YULE, TENA PANA TOFAUTI YA HUDUMA BALI BWANA NI YEYE YULE. TENA PANATOFAUTI YA KUTENDA KAZI BALI MUNGU NI YEYE YULE AZITENDAYE KAZI ZOTE KATIKA WOTE. LAKINI KILA MMOJA HUPEWA UFUNUO WA ROHO KWA KUFAIDIANA. MAANA MTU MMOJA KWA ROHO HUPEWA NENO LA HEKIMA NA MWINGINE NENO MAARIFA BALI ROHO NI YEYE YULE …….

Karama aliyenayo mwenzako ndiyo uhitaji wako, HUduma alie nayo mwenzako ndio unayohitaji ilikupiga hatua, lakini pia mnaweza makafanana huduma lakini utendaji kazi ukatofautiana jua hivi ulipewa kwaajili ya wengine. Utofauti wa utendaji kazi wa huduma ni kwaajili ya kusaidiana na kuhudumiana kwa wenye huduma inayifanana naam na wenye huduma zingine pia. Niruhusu nitumie mfano wa kipaji cha michezo kuelezea zana hii. Kwenye mchezo wa mpira wa miguu, kuna makundi matatu (unaweza kuyagawanya Zaidi ya hapo) kundi la kwanza ni wachezaji, wawezeshaji na la mwisho mashabiki au wanufaikaji wa mchezo. Maana namna aliyepewa inawezekana isimfaidie yeye bali waliomzunguka. Kumbuka kazi ya karama ni kufaidiana na sio kumnufaisha mwenye karama au kipaji. ( kuna marupurupu na Lengo, kuwa makini)

Hahahaha mkono hauwezi kujishika mwenyewe utashikwa na mkono mwingine, Tunahitajiana sana.

1korintho12:12

Ukiona unajimwamba fai kama asemavyo rafiki wa seremala, pstr Raphael lyela, ujue kabisa ndio mwanzo wa kunyauka kwako, na sifa pekee itakayokubeba na itakayobebwa ni ya Jana yako huku leo yako ikijaribu kufuta kwa bidiii sifa njema uliyoitengeneza jana, kwa karama na kipaji alichokupa MUNGU.

Mkono unahitaji kusafishwa na mkono mwingine, huwezi kujisafisha mwenyewe, Ndivyo ilivyo mwalimu anamwihitaji mwalimu iliawe bora Zaidi na kufaa mbele za MUNGU, Nabii anamuhitaji pia Nabii mwingine iliakue na kuongezeka katika kimo akimpendeza MUNGU na wanadamu, kama jicho linavyomuhitaji mtu mwingine kumtazama na ilikuona kama kuna kuna uchafu au mdudu ili mikono ifanye kazi yake vyema.

No comments:

Post a Comment